YOHANE 1:1-5
Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.
Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.
Leave a comment